Kiongozi wa Wanafunzi 46 wa Skuli mbali mbali za Sekondari kutoka Nchini marekani waliopo Kiwengwa Zanzibar Bwana Criss Backam akimuelezea Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi uwepo wao wa kujitolewa katika ujenzi wa skuli kupitia mradi wa Give Kutoka nchini humo.Kati kati yao ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mheshimiwa Ali Juma Shamhuna.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akiwashukuru na kuwapongeza Wanafunzi wa skuli mbali mbali za Sekondari Nchini Marekani ambao wapo Zanzibar wakijitolea katika mradi wa ujenzi wa skuli mpya ya Kiwengwa.
Balozi Seif, Mkewe Mama Asha Suleiman Iddi na Waziri wa Elimu Mh. Ali Juma Shamhuna wakiwa katika picha ya pamoja na Wanafunzi wa kujitolea kutoka skuli mbali mbali za Sekondari Nchini Marekani hapo Kiwengwa Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Baadhi ya msaada wa Kompyuta zilizokabidhiwa Wizara ya Elimu kwa ajili ya Skuli za Zanzibar zikitoka Rotary Klabu ya Kimataifa ya Mji wa Seattle Nchini Marekani.






Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...