Picha ya Marehemu Sheila Leo Haule (Rachel) ikiwa pembeni ya Jeneza lake mchana wa leo wakati wa kuagwa kwa mwili wake,kwenye viwanja vya Leaders Club,Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Wacheza filamu hapa nchini,wakiwa pembeni ya Jeneza la Mpendwa wao Sheila Leo Haule (Rachel) aliefikwa na umauti hivi karibuni.
Bw. Saguda ambaye ndie alikuwa mchumba wa Marehemu akilia kwa uchungu huku akiliwazwa na nduguye.
Mwenyekiti wa Bongo Movie,Steven Nyerere akilia kwa uchungu.
Sehemu ya wacheza filamu wa Bongo Movie wakilia kwa uchuku kwa kuondokewa na Mwenzao,Marehemu Sheila Leo Haule (Rachel) wakati wa shughuli ya kuaga mwili wake iliyofanyika mchana wa leo kwenye viwanja vya Leaders Club,Jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...