Meneja uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania, Salum Mwalim, akizungumza na waandishi wa habari (Hawapo pichani) wakati wa kutangaza siku ya kukabidhi zawadi za washindi wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Pamoja nae katika picha, wa kwanza kutoka kushoto ni Ofisa Matukio na Udhamini wa Vodacom Tanzania, Ibrahim Kaude, Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura.

Bingwa wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara 2013/2014 timu ya Azam FC itakabidhiwa kitita chake cha zawadi Sh 75 Milioni Mei 27 mwaka huu kutoka kwa mdhamini wa ligi hiyo kampuni ya huduma za mawasiliano ya simu za mkononi nchini ya Vodacom.

Aidha, pamoja na Azam fc, Vodacom itakabidhi pia zawadi za fedha kwa Yanga, Mbeya City na Simba waliomaliza msimu katika nafasi ya pili hadi ya nne.

Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim amesema tayari maandalizi ya tukio hilo litakalohusisha chakula cha jioni yameshakamilisha kwa kiasi kikubwa na kinachoendela sasa ni maandalizi ya mwisho ikiwemo kusambaza mialiko.

Mwalim amesema tukio hilo hilo litafanyika kwenye ukumbi wa JB Belmonte uliopo kwenye jengo la Golden Jubilee jijini Dar es salaam na kuwataka washabiki wa soka nchini kuaka mkao w akuhushudia tukio kubwa na la aina yake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...