Umoja wa Waendesha Pikipiki wilayani Temeke ( UWAPITE) umekutana na kufanya mkutano wao mkuu leo katika ukumbi wa CCM kata 14 Temeke. Mgeni rasmi alikuwa ni Mjumbe wa NEC Ndg. Phares Magesa, ambaye aliwataka wanaboda boda hao kutii sheria na taratibu zote kama walivyotakiwa na Mamlaka husika, pia Ndg. Magesa aliwaasa wanabodaboda hao kuimarisha Umoja wao ili waweze kufanikiwa kufikia malengo yao. Ndg. Magesa aliahidi kufikisha katika Mamlaka husika mambo mbalimbali ambayo wanabodaboda hao waliomba ikiwa ni pamoja na suala la utaratibu wa kuingia mjini na aliwaomba wawe na subira wakati mambo hayo yanashugulikiwa. Mkutano huo pia ulihutubiwa na viongozi wengine toka taasisi mbalimbali akiwemo Afisa Usafirishaji wa Mkoa, Kamanda wa Polisi, Sumatra, Bima (NIC) na wawekezaji toka kampuni ya Yamaha ambao wanatoa mikopo nafuu kwa wanachama wa Chama hicho.
Wanachama wa Chama Cha Waendesha Pikipiki Temeke wakisiliza hutuba mbalimbali zilizotolewa.
Mgeni rasmi Ndg.Phares Magesa akitoa nasaha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...