Mhe. Naimi Aziz, Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia ( wa nne kutoka kulia) akiwa na baadhi ya wanariadha wa Mbio ndefu kutoka Tanzania waliowasili jijini Addis Ababa siku ya Alhamisi tarehe 1/5/2014, kwa ajili ya kufanya mazoezi ya nguvu ya kujiandaa na Mashindano ya Jumuiya ya Madola yatakayofanyika nchini Scotland mwezi wa Saba mwaka huu. Wizara ya Michezo ya Ethiopia imeamua kutoa makocha watatu ambao watasaidiana na kocha Shabaan Bayu katika kukinoa kikosi hicho. Aidha, mwanariadha mashuhuri wa Ethiopia Haile-mariam Gabresilas na ye amepangiwa kukutana na kikosi hicho.
Home
Unlabelled
WANARIADHA WA MBIO NDEFU WAWASILI ADDIS ABABA KWA AJILI YA MAZOEZI YA KUJIAANDAA NA MASHINDANO YA JUMUIYA YA MADOLA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Fanyeni mazoezi mkitegemea zawadi ya juu kabisa.
ReplyDeleteWale wanariadha wa POLISI waliofanya vizuri ktk mashindano ya kikand kule nchini Namibia wamo pia?
ReplyDelete