Meya wa Manipaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda amewataka wananchi wa Manispaa yake na nchini kote kuwasaidia watoto yatima na wasiojiweza ili kupunguza tatizo la watoto wa mitaani na mayatima ambao wamekuwa wakiongezeka kila siku jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa futari aliyoiandaa kwa wananchi wa Manispaa yake, viongozi wa Kiserikali na kidini, Dar es Salaam juzi Meya huyo alisema kuwa Manispaa yake ni kubwa na hivyo endapo watu watachukua maamuzi ya kusaidia watoto hao basi tatizo hilo litakuwa limepungua kwa kiasi kikubwa katika Manispaa hiyo na jijini kwa ujumla.

“Wito wangu kwenu tuwasaidie watoto yatima na wanaoishi kwenye mazingira magumu katika Manispaa yetu ili kuondoa tatizo hili la watoto wanaozagaa mitaani kwani nao wana haki kama walivyo watoto wengine wenye wazazi na wanaoishi kwenye mazingira mazuri. Nazungumza hili kwa kuwa hili ni tatizo sugu katika Manispaa yetu.” Alisema.

Aidha aliwahakikishia wananchi hao kuwa Manispaa itaendelea kufanya kila inachoweza kuhakikisha inaboresha hali ya maisha ya wananchi wake bila kujali itikadi za kisiasa wala kidini ili kuondoa umasikini kwa wananchi hao. Pia alisema Manispaa itaendelea kusimamia kampeni yake ya kuweka mazingira safi ya Manispaa kwa kuhakikisha inatimiza malengo yake iliyojiwekea.

“Niseme kuwa sisi (Manispaa) ndio tunaoondoa taka kwa asilimia 75 hapa jijini, nawapongeza Madiwani wangu kwa kusimamia vema kampeni mbalimbali tunazozianzisha katika Halmashauri yetu.” Alisema

Kwa upande wake Shehe wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Saluma aliwahimiza waumini wa dini ya Kiislam kuzidisha ibada katika kumi hili la mwisho la mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan na kusema kuwa endapo muumini atakutwa na usiku wa lailatul qadir basi ni sawa na kufunga miezi 1000 ambayo ni sawa na miaka 83.
Shehe wa Wilaya ya Kinondoni, Alhaj Mohamed Mwenda (mbele) akiowaongoza waumini katika swala ya Magharibi, kabla ya kupata futari iliyoandaliwa na Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda kwa wananchi wa Manispaa yake, viongzoi wa kiserikali na kidini, Dar es Salaam jana. Kutoka kulia (mstari wa mbele) ni Shehe Mkuu wa Tanzania, Mufti Issa Shaabn Bin Simba, Imam wa Msikiti wa Alfarouq, Mwita Kambi, Shehe wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum, Meya wa Manispaa hiyo, Yusuph Mwenda, viongozi mbalimbali wa dini na wa kiserikali.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda (kulia) akiwaongoza wageni mbalimbali kupakua futari aliyoindaa kwa wananchi wa Manispaa yake, viongozi wa kiserikali na wa kidini, Dar es Salaam jana. Kulia kwake ni Shehe wa Dar es Salaam Alhad Mussa Salum.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda (wa pili kushoto0 akipata futari pamoja na Shehe Mkuu wa Tanzania, Mufti Issa Shaaban Bin Simba (kushoto kwake), Shehe wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum (kulia) na Shehe wa Wilaya ya Kinondoni, Alhaj Mohamed Mwenda wakati wa futari aliyoiandaa kwa wananchi, viongozi wa kiserikali na kidini wa Manispaa yake, jijini jana.
Mbunge wa Kinondoni, Iddi Azzan (kulia) akibadilishana mawazo na Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda (wa tatu kushoto) wakati wakipata futari iliyoandaliwa na Meya huyo kwa wananchi, viongozi wa kiserikali na kidini wa Manispaa yake, Dar es Salaam jana. Wengine ni Shehe Mkuu wa Tanzania, Mufti Issa Shaaban Bin Simba (wa tatu kulia), Shehe wa Mkoa wa Dar es Salaam Alhad Mussa Salum (wa pili kulia) na viongozi wengine wa kidini na kiserikali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...