Mitandao jamii imekuwa moja ya nyenzo imara kabisa ya kujitangaza na kuwafikia walengwa wengi kwa uharaka na mapana zaidi kwa njia ya mtandao. Jiulize swali dogo tuu, je kwa siku za karibuni umekuwa ukitumia njia gani kufahamu juu ya bidhaa au huduma fulani.

Je kwa kutumia tangazo la kwenye TV au Radio ambapo hauna uhakika hata saa ngapi wataonesha tangazo unalohitaji? Au kwa kupitia gazeti ambapo wengi wetu sasa inapita hata mwezi bila kusoma gazeti lililochapishwa? Au ni mara ngapi umetumia muda wako kusoma lundo la emails kwenye sanduku la email za matangazo (Junk emails)?

Matumizi ya facebook kwa Biashara

Siku hizi watu wamebadilika sana, wateja hupendelea kutafuta huduma toka mahali ambapo wanapata taarifa zote kwa upamoja tena pindi wanapohitaji, baadhi ya njia watumiazo kwa sana ni kama; kwa kutumia mitambo ya utafutaji (search engines) au toka kwa marafiki zao walio kwenye mitandao jamii (Social networks). Na huko ndiko kunakoshibisha njaa ya huduma na kujibu maswali yao yote.

Je wewe ni mmoja wa watoa huduma wanaoshibisha njaa ya taarifa za huduma au kujibu maswali ya wateja? Facebook siyo sehemu ya kupotezea muda kama wengi wanavyofikiria, pia siyo sehemu ya vijana peke yake na wala siyo sehemu ya kukimbiwa na wafanyabiashara makini.Facebook ni sehemu inayounganisha watu pamoja, na wewe kama mfanyabishara makini,Facebook ni sehemu sahihi itakayokuwezesha kujitanua na kukutana na wateja wengi wa sasa na wa baadae.

 Twende kazi, ili kuwasaidia wafanyabiashara na Wakurugenzi juu ya matumizi thabiti ya Facebook kibiashara, Dudumizi Technologies imeandaa kitabu kifupi juu ya matumizi ya Facebook kwa biashara,kitabu hiki kimelenga na kujikita moja kwa moja kukuongoza kwenye kila kitu muhimu unachotakiwa kukifahamu kwenye matumizi thabiti ya Facebook kwa biashra yako. Utakapomaliza kitabu hiki, basi utakuwa na uelewa mzuri siyo tuu kuhusu mitandao Facebook yenyewe kama Facebook, bali mahusiano yake na biashara yako
 



Kwa makala zaidi za IT fuatilia kurasa wetu wa Facebook http://www.facebook.com/dudumizi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...