Na Editha Karlo wa Globu ya Jamii,Kigoma

KAMANDA wa Kikosi cha Jeshi la kujenga Taifa (JKT) 824 KJ cha Kanemwa wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma Luteni Kanali Erasmus Bwegoge ameomba Halmashauri ya wilaya hiyo kutilia mkazo na kuhitimisha mchakato wa kupata hati miliki ya maeneo ya kikosi hicho ili kuondoa uwezekano wa wananchi kuvamia maeneo hayo jambo ambalo linaweza kuzua migogoro na kuhatarisha mahusiao baina ya Jeshi na wananchi.

Luteni kanali Bwegoge ametoa ombi kwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Luteni kanali mstaafu Issa Machibya wakati wa mahafali ya nne ya kuhitimu mafunzo ya jeshi kwa mujibu wa sheria .

''Mgeni rasmi tunaomba Halmashauri yetu ya Kakonko suala la kupata hati miliki ya maeneo ya kikosi chetu hiki,hii itatusaidia sana kuondoa migogoro ya ardhi baina ya wananchi na jeshi,pia itasadia kutokuwepo na wananchi wanaovamia katika maeneo ya jeshi''alisema.

Alisema kuwa pamoja na kuwepo kwa changamoo hiyo ya ardhi kikosini hapo pia kuna changamoto za huduma bora za afya alisema jumla ya vijana 1127 wa oparesheni ya miaka 50 ya muungano wamehitimu mafunzo hayo ambao ni wahitimu wa kozi ya ualimu na wale waliomaliza kidato cha sita .

Kwa upande wake mwakilishi wa mkuu wa Jeshi la kujenga Taifa nchini(JKT) Meja Abdulrahmani Dachi na mgeni rasmi katika maafali hayo Mkuu wa M koa wa Kigoma Luten Kanali mstaafu Issa Machibya wamewataka vijana hao kutumia mbinu walizojifunza kudumisha ulinzi na usalama wa nchi pamoja na kuhamasisha shughuli za maendeleo katika jamii na si kulihujumu Taifa kwa namna yeyote.

''Muende mkawe mfano wa kuigwa katika jamii pia mtumie mbinu mlizofundishwa katika kudumisha ulinzi na usalama wa nchini pia mkawe mfano katika shughuli za maendeleo katika jamii''alisema Mkuu wa Mkoa
Baadhi ya wahitimu wa mafunzo ya Jeshi la kujenga Taifa katika kikosi cha 824 KJ Kanembwa wakiwa tayari kwaajili ya Gwaride.
Wahitimu wakipita mbele ya mgeni (hayupo pichani)Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kanali mstaafu Issa Machibya rasmi kwa mwendo wa pole.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. I like kanembwa, kikosi kilichonitoa uraia salute kwenu

    ReplyDelete
  2. Nitakupenda daima Kanembwa, 824ilinitoa uraia salute kwenu nyote

    ReplyDelete
  3. I like kanembwa, kikosi kilichonitoa uraia salute kwenu

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...