SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limeanza ukarabati katika Uwanja wa Kaitaba uliopo mkoani Kagera kuanzia Januari 12,2015.
Rais wa TFF, Jamal Malinzi alisema kuwa kutokana na ukarabati huo tayari Kagera Sugar imeshaomba kutumia Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza kwa ajili ya mechi zake za nyumbani. Katika hatua nyingine, Malinzi alisema kutokana na kikao cha Kamati ya Utendaji cha FIFA kilichokutana hivi karibuni kiliweka wazi kila Mwanachama wa FIFA ataendelea kupata dola za kimalekani 600,000 kwa mwaka kwa ajili ya maendeleo ya Soka.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...