Katibu mtendaji wa taasisi isiyo ya kiserikali inayojishughulisha na masuala ya maendeleo ya jamii (CODERT), Hellen Kayanza akifafanua jambo wakati wa shughuli iliyoandaliwa na Benki ya Exim jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, kuadhimisha siku ya wanawake duniani ambayo husherehekewa Machi 8 kila mwaka. 

Wakati wa shughuli hiyo wafanyakazi wa kike wa benki hiyo walitoa wito kwa wanawake nchini kutumia maadhimisho ya mwaka huu kutokomeza ukatili dhidi ya wafanyakazi wa ndani. Wanaotizama ni Meneja mwandamizi wa kitengo cha rasilimali watu wa benki ya Exim, Joan Mbakileki na Mkuu wa matawi wa benki hiyo, Elizabeth Mayengoh.
Mkuu wa matawi wa Benki ya Exim, Elizabeth Mayengoh (kulia), akikabidhi zawadi kwa Katibu mtendaji wa taasisi isiyo ya kiserikali inayojishughulisha na masuala ya maendeleo ya jamii (CODERT), Hellen Kayanza (wa pili kulia) wakati wa shughuli iliyoandaliwa na Benki ya Exim jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki kuadhimisha siku ya wanawake duniani ambayo husherehekewa Machi 8. 

Wakati wa shughuli hiyo wafanyakazi wa kike wa benki hiyo walitoa wito kwa wanawake nchini kutumia siku hiyo kutokomeza ukatili dhidi ya wafanyakazi wa ndani. Wanaotizama ni Mkuu wa matawi wa benki hiyo, Agnes Kaganda (kushoto) na Meneja mwandamizi wa kitengo cha rasilimali watu wa benki ya Exim, Joan Mbakileki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...