Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Mhe. Mohamed Chande Othman akiwa na Mlinzi wa Usalama katika Umoja wa Mataifa, Afisa Ally Baruti kutoka Tanzania, Mhe. Jaji Mkuu yupo hapa Umoja wa Mataifa akiongoza Jopo Huru la Wataalam wanaopitia na kuchambua taarifa mpya kuhusu kifo cha Bw. Dag Hammarskjold ambaye aliwahi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon alimteua Mhe. Jaji Mkuu kuongoza jopo hilo mwezi uliopita, Wajumbe wengine ni Bw. Kerryn Macaulay kutoka Australia na Bw. Henrik Ejrup Larsen kutoka Denmark.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...