Kamanda wa
Polisi wa kikosi cha usalama Barabarani Mohammed Mpinga,akizungumza na
waandishi wa habari hawapo pichani ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya
waandishi wa habari waliohudhuria mkutano
na Kamanda wa Polisi wa kikosi cha usalama barabarani Mohammed Mpinga jijini Dar leo.(Picha na Emmanuel Massaka).
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.
KIKOSI cha Usalama Barabarani kimesema wanazifuta leseni zote kwa madereva waliosababisha ajali kwa uzembe zikiwemo ajali za hivi karibuni.
Hayo ameyasema leo jijini Dar es Salaam,Kamanda wa Polisi wa Kikosi cha Usalama Barabarani,Mohamed Mpinga,amesema katika kukabiliana na wimbi la ajali ni pamoja na kufuta leseni kwa madereva wazembe ambao wanasababisha ajali.
Mpinga amesema ajali za hivi karibuni zimesababishwa na uzembe wa madereva, hivyo ni lazima kufuta leseni zao na hawatakiwi kufanya kazi yoyote ya udereva nchini pamoja na kuweka katika tovuti taarifa zao ili watu wengine wasiwachukue.
Amesema katika usafiri wa mabasi watakuwa wanaangalia muda kutoka sehemu hadi nyingine na basi ambalo litakuwa mbele ya muda uliopangwa katika eneo husika hatua zitachukuliwa.
Mpinga ametoa pole kwa wafiwa waliopoteza maisha katika ajali za hivi karibuni na kusema wale wote waliosababisha ajali hizo watafutiwa leseni na hatua zingine kufuta ili madereva wengine wasifanye makosa hayo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...