Mkuu wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo akimpokea Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, WAMA, Mama Salma Kikwete wakati alipowasili kwenye uwanja wa mpira wa Shule ya Sekondari Nyamisati iliyoko wilayani Rufiji kwa helicopter tarehe 2.5.2015. Mama Salma alikwenda Rufiji kwenye tamasha la Elimu ya Afya ya Uzazi kwa vijana katika Shule ya Sekondari ya WAMA-Nakayama ambayo inamilikiwa na Taasisi ya WAMA ambapo Mkuu wa Mkoa wa Pwani alikuwa Mgeni Rasmi.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete akifuatana na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo (kulia) na Makamu Mwenyekiti wa WAMA Mheshimiwa Zakhia Meghji (kushoto) wakiingia kwenye ukumbi wa Shule ya Sekondari Nwama-Nakayama kuhudhuria Tamasha la Elimu ya Afya ya Uzazi kwa Vijana wa Shule hiyo tarehe 2.5.2015.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...