Wafanyakazi wa Ecobank Tanzania wakikata keki kwa pamoja na wateja wa benki hiyo Bw. Betwel Usio (Katikati) na Anna Swai (wa kwanza kushoto) kuashiria uzinduzi rasmi wa wiki ya huduma kwa wateja katika hafla iliyofanyika kwenye tawi la benki hiyo la Sokoine jijini Dar es salaam.
Meneja wa benki tawi la Sokoine Bi. Anna Chimalilio akimlisha keki moja ya wateja wa benki hiyo Bw. Betwel Usio wakati wa uzinduzi wa wiki ya huduma kwa wateja katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika kwenye tawi la benki hiyo la Sokoine jijini Dar es salaam.
Wafanyakazi wa Ecobank Tanzania tawi la Sokoine wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa uzinduzi wa wiki ya huduma kwa wateja katika hafla ya uzinduzi uliofanyika kwenye tawi la benki hiyo la Sokoine jijini Dar es salaam.
Ecobank Tanzania imezindua rasmi wiki ya huduma kwa wateja kwa mara ya kwanza nchini ambayo itaadhimishwa mara moja kila mwaka. Kampeni hiyo iliyoanza rasmi siku ya leo ni njia mojawapo ya benki hiyo kutoa shukrani kwa wateja wake pamoja na kudhihirisha uthamini wao kwa wateja hao.
Kauli mbiu ya mwaka huu ikiwa ni “Tunashukuru” imezinduliwa rasmi leo kwenye tawi la Sokoine la benki hiyo lililopo barabara ya Sokoine (jengo la Karimjee Jivanjee) na itatumika kipindi kizima cha siku 4 za kampeni hiyo.
BOFYA HAPA KWA HABARI KAMILI
BOFYA HAPA KWA HABARI KAMILI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...