SIKU
YA MOYO, WANANCHI KUPIMWA SHINIKIZO LA DAMU BURE.
KATIKA kuazimisha siku ya afya ya Moyo Duniani Hospitali ya
Taifa Muhimbili-MNH- leo itatoa huduma ya upimaji wa shinikizo la damu bure
pamoja na kuwashauri wale watakaopatikana na tatizo hilo.
Akizungumza
na waandishi wa habari kuhusu siku ya afya ya moyo Duniani ambayo huazimishwa
Septemba 29 kila mwaka , Daktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo Tulizo Shemu kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kitwete amesema magonjwa ya moyo
yanachangia asilimia 31 ya vifo vyote vinavyosababisha takribani watu MIlioni
17. 3 kufa kila mwaka .
Inasadikika itakapofika mwaka 2030 zaidi ya watu Milioni 25
watakuwa wanapoteza maisha kutokana na maradhi hayo hasa katika nchi zilizo na
uchumi wa chini na kati.
Siku ya afya ya moyo Duniani hutoa fursa kwa watu wote
Duniani kuazimisha kwa vitendo katika kujilinda na janga la magonjwa ya moyo na
mishipa ya damu ambayo yanachangia vifo vingi .
Dokta Shem ametaja baadhi ya visababishi vinavyochangia
magonjwa ya moyo kuwa ni matumizi ya tumbaku, chumvi , pombe, vyakula vyenye
mafuta, kutofanya mazoezi , unene uliokithiri , kutotibu ugonjwa wa kisukari na
kuwa na mafuta mengi kwenye damu.
Kauli
mbiu ya mwaka huu ni kuweka mazingira mazuri ya afya bora ya moyo katika sehemu
zetu tunazofanyia kazi kwa kuhakikisha kila mtu anatoa mchango katika kujenga
afya bora ya moyo ili kupunguza visababishi vinavyochochea magonjwa hayo.
Daktari Bingwa wa magonwa ya moyo, Dk Tulizo Shemu (kulia) wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) akizungumza na waandishi wa habari katika taasisi hiyo kuhusu siku ya afya ya moyo duniani ambayo inafanyika Septemba 29, kila mwaka.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo nchini, Dk Tatizo Wane (kulia) wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) akizungumza na waandishi wa habari katika taasisi hiyo kuhusu siku ya afya ya moyo duniani ambayo inafanyika Septemba 29, kila mwaka. Kesho watu watapimwa bure shinikizo la damu na watakaopatikana na tatizo hilo watapewa ushauri wa bure. Pia siku ya kesho (Septemba 29, 2015) Taasisi hiyo itagawa vepeperushi, majarida na CD zinazozungumzia magonjwa ya moyo.
Baadhi ya waandishi wa habari.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...