Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma Bw. HAB Mkwizu anasikitika kutangaza kifo cha Bw. Yakalawa
Kondo – Msaidizi wa Ofisi Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa
Umma (Pichani) kilichotokea tarehe 21.09.2015 saa 3 usiku katika Kituo cha Afya
cha Vijibweni - Kigamboni. Mazishi yalifanyika tarehe 22.09.2015 saa 10 jioni
katika makaburi ya Tungi Shule – Kigamboni.
“Mungu
ailaze Roho ya Marehemu Mahala Pema
Peponi, Amen”
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...