Pr. Mwakabonga akiongoza ibada ya kumbukumbu ya marehemu Godfrey Mbiu
Mngodo iliyofanyika siku ya Jumamosi Octoba 31, 2015 Columbus, Ohio nchini
Marekani na kuhudhuriwa na ndugu, jamaa na marafiki wakiwemo wafanyakazi wa
kituo cha utangazaji Sauti ya Amerika idhaa ya Kiswahili (VOA). Marehemu
Godfrey Mbiu Mngodo aliaga Dunia Tarehe 11 Septemba, 2015 Dar es Salaam na
kuzikwa Tanga. Godfrey Mbiu Mngodo amefanya kazi katika sehemu
mbalimbali kama Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD), Voice of America,
wizarani na kituo cha Channel Ten ameacha watoto 10 na wajukuu 14. PICHA NA
KWANZA PRODUCTION/VIJIMAMBO
Mmoja ya mtoto wa marehemu Michael Mngodo akiwa na mwanae Alvin
wakifuatilia ibada ya kumbukumbu ya mpendwa baba yake marehemu Godfrey Mbiu
Mngodo iliyofanyika siku ya Jumamosi Octoba 31, 2015 Columbus, Ohio nchini
Marekani.
Familia ya Mngodo ikifuatilia Ibada.
Pr. Mwakaboma akifanya maombi kwa wanafamilia.
Michael Mngodo akisoma wasifu wa mpendwa baba yake. Kulia ni mtoto wake
Alvin.
Ndugu, jamaa na marafiki wakifuatilia ibada. Kwa Picha zaidi bofya HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...