Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue atafanya ziara katika Hospitali ya Taifa Mhimbili Kesho Jumatatu (23 Novemba, 2015) kuanzia majira ya saa nne asubuhi.

Ziara hiyo ni kwa ajili ya kukagua utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyeagiza fedha zilizochangwa ajili ya hafla ya wabunge zitumike kununulia vitanda vya wagonjwa katika hospitali hiyo.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasilino, IKULU

20 Novemba, 2015

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Sawa mkuu tuko nawe. Hii safi sana. Mungu awatie nguvu na kuwalinda.

    ReplyDelete
  2. Wazo zuri sana naipongeza serikali.kwa hlo

    ReplyDelete
  3. hizi press releases zingekuwa na heading na kumbukumbu namba ingekuwa vema zaidi

    ReplyDelete
  4. KWA MARA YA KWANZA KTK HISTORIA YA TANZANIA, AKA BONGO LAND, BAADHI YA WABUNGE WANAHAHA NA KUOMBA WASICHAGULIWE KUWA MAWAZIRI, KWANI HAPA KAZI TU!

    ReplyDelete
  5. HAYO NDIYO MABADILIKO YA UKWELI, KWA KWELI NI VITENDO TU SIYO MANENO, KURA ZETU ZINATENDEWA HAKI. HONGERA SANA RAIS, TUNAKUOMBEA. WATAPIGANA NAWE LAKINI HAWATASHINDA MAANA MUNGU YUKO PAMOJA NAWE. AMINA

    ReplyDelete
  6. UFUATILIAJI NDIO TATIZO KUBWA NCHI HII LAKINI TUMEANZA VZRNA RAIS AMEONYESHA MFANO NA VIONGOZI WENGINE WAENDE TEMEKE NA MWANANYAMALA TUSIMNGOJE RAIS TU PEKE YAKE ATACHOKA. WAKUU WA MIKOA WILAYA HARUWASIKII!!!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...