Ndege ya uzinduzi ya Shirika la Ndege la Etihad ikipokelewa na magari ya zimamoto ambayo yalimwaga maji kuashiria uzinduzi rasmi wa Safari za ndege kati ya Rabat na Abudhabi.
Safari kati ya Abu Dhabi na Morocco kufikia tisa kwa wiki
Shirika la ndege la Etihad lazindua rasmi huduma zake za ndege baina ya Abu Dhabi na Rabat, Morocco, ikiwa ni kituo chao cha pili nchini humo.
Ndege ya uzinduzi iliwasili mchana wa leo uwanja wa ndege Sale-Rabat na kupokelewa na mzinga wa maji kama ilivyo desturi ikifuatiwa na wageni rasmi kuwasili, wakiwemo; Lahcen Haddad (Waziri wa Utalii Morocco), na Balozi wa UAE kwa Morocco, Mh. Al Asri Saeed Al Dhaeri.
Huduma hii itakayopatikana mara mbili kwa wiki kupitia ndege aina ya Airbus A340-500 itakuwa yakipekee baina ya Rabat na Abu Dhabi. Tayari kukiwa na safari baina ya Abu Dhabi na Casablanca, shirika litafikisha jumla ya safari tisa kwa wiki kwenda nchini Morocco
Ndege ya uzinduzi (EY615) kwenda Rabat ilibeba msafara ulioongozwa na Khaled Al Mehairbi, Makamu Rais Mambo ya Serikali na Siasa za Anga. Uwakilishi huu ulijumuisha Kapteni Salah Awadh Alfarajalla, Makamu Rais Usalama na Maaendeleo ya Waendesha Ndege Kitaifa; Hareb Mubarak Al Muhairy, Makamu Rais Mambo ya Mashirika na Kimataifa; Ali Al Shamsi, Makamu Rias Operesheni za Kitovu cha Abu Dhabi; Joost Den Hartog, Kaimu Makamu Rais wa Mauzo Duniani; na Amer Khan, Makamu Rais Mashariki ya Kati na Africa Kaskazini.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...