Mwigizaji bora wa kike wa Komedi Swahiliwood Salma Jabu ‘Nishabebee’ anawashukru wadau wote wa tasnia ya filamu kwa ujumla wake kutokana na mchango wao ambao wamempa kupitia kazi zake ambazo ameshiriki katika kuigiza na kutayarisha  filamu zaidi ya 8 chini ya kampuni yake ya Nisha’s Film Productions. 
Akiongea na wanahabari msanii huyo ambaye ana sifa za kimataifa amesema kuwa baada ya filamu yake ya Kiboko Kabisa inamfungulia mwaka na kuwa kazi yake ya awali kuingia sokoni leo siku ya Ijuma,  anasema kuwa amejifunza mengi na anatoa shukrani kwa wadau wa filamu ambao wamekuwa bega kwa bega katika kuhakikisha anasonga mbele kisanaa. 
“Nawashukru wote wanahabari jamaa zangu hata wale ambao wamekuwa wakinishauri kupitia njia mbalimbali, kila mtu kwangu ana mchango mkubwa sana naheshimu hilo kwa kila mtu kwa nafasi aliyo nayo na kuhakikisha wanafanya jambo kubwa kwa ajili yangu Asanteni sana na Mungu awabariki,”anasema Nisha. 
Aidha msanii huyo ameamua kuanzisha utaratibu wa kutoa taarifa za maendeleo ya kazi yoyote ambayo atakuwa akiifanya na taarifa kuwafikia wapenzi wa filamu nchini nzima na kuwa ndio njia ya wasanii kujenga mahusiano mema na watazamaji wao ambao kuna wanataka kujua maisha ya wasanii ya kawaida nje ya uigizaji lakini si rahisi.
 Anawashukru sana wapenzi wa filamu Swahiliwood ambao siku zote wamekuwa wakimuunga mkono katika kazi zake ambazo zimepita kama vile Gumzo, Mtaa kwa Mtaa na leo hii anaingia na filamu ya Kiboko Kabisa sinema hiyo imewashirikisha wasanii wakali katika tasnia ya filamu King Majuto, Nishabebee, Ben Blanco, Mzee Jengua.
Filamu ya Kiboko kabisa imeingia sokoni siku ya ijumaa ya tarehe 29.January . 2016 na inapatikana nje nzima anaomba kila mwananchi ajenge tabia ya kununua kazi ambazo ni halali na si kazi bandia ambazo zinashusha maisha ya wadau wa filamu.
 Nisha ambaye kwa sasa ni kipenzi cha watoto na wapenzi wa komedi anasema kuwa anatamani kumfikia kila mtu kwa kuongea naye ana kwa ana lakini si rahisi waamini kuwa anawajali ni rafiki wa kweli kwa kila raia wa Tanzania kwani anaamini wote ni ndugu zake.
Nisha mwigizaji bora wa Kike kushinda tuzo za action & cut Views Choice Awards (ACVA 2013/2014) amekuwa ndio msanii pekee ambaye kila kazi yake anapoifanya na kuingia sokoni huwa gumzo kama jina la moja ya filamu ambayo aliwahi kutengeneza ya Gumzo. 
Kwa mwaka huu Nisha amesema kuwa katika sherehe zake muhimu ambazo huzifanya atahakikisha anakula pamoja na watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi, akina mama wajane na watu walio katika shida kubwa kwenye maisha ya kawaida.
Aidha msanii huyo anachukua muda kuwashukru wanahabari kwa kuwataarifu wapenzi wa kazi zake kwani anaamini bila wao wana mchango mkubwa sana hadi alipofika na anaendelea kuwaheshimu na kutoa ushikiano kwao katika kuhabarisha jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...