Raia wa Ujerumani (kulia) ambaye jina lake halikupatikana mara
moja, ametiwa na mbaroni na Jeshi la  Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa tuhuma za kutaka kuitoroka  familia yake katika  Hoteli ya Cate Dar es Salaam. Raia huyo alikuwa nchini na mkewe mwenye asili ya Afrika katika kipindi cha msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka. Alijaribu kumtoroka mkewe na mtoto (4) na kuwaacha wakidaiwa deni la sh. 315,000 baada ya kile kilichodaiwa kuzuka ugomvi baina yao.

 Mtoto wao (4) akisaidiwa kupandishwa katika Gari




 Raia wa Ujerumani huyo akitaka kuruka toka katika Gari la Polisi
 Mke wa Raia wa Ujerumani wa pili kulia akiwa anaingia katika Gari kuelekea katika Kituo cha Polisi cha Msimbazi Dar es Salaam na wapili kulia ni kaka wa mwanamke wa Raia wa Ujerumani
Wananchi wakifuatilia kwa karibu tukio hilo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Nimeguswa sana na habari hii. Sijui undani wake, lakini kwa vyovyote vile, namsikitikia huyu mtoto. Katika hali kama hizi, watoto ni wahanga moja kwa moja.

    ReplyDelete
  2. Heee, mtoto naye anaenda keko!!

    ReplyDelete
  3. weh! Mjerumani vipi? umewakimbia ffu-ughaibuni kina ras makunja unakuja kupewa kibano na ffu wa bongo,mkeo na mtoto rudi nao huko huko na kina ras wanakusubiri kwa hamu

    ReplyDelete
  4. Namwonea huruma mtoto, yeye ni innocent victim wa ugomvi wa wazazi wake!

    ReplyDelete
  5. Wazungu jamani tuwe nao makini, ukishuka bongo jiweke sawa pia..wanadharau, inauma zaidi kwa mtoto wake hata hajali. Kisaikolojia kamuharibu sn. Alafu nani kumuambia amshike afande bega, afande nae kasikilizia. Ingekuwa Ujeruman mwafrika angemshika polis mzungu???

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...