JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI
![]() |
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.
KUHUSU UPOTOSHWAJI WA TAARIFA ZILIZOANDIKWA NA
GAZETI LA MWANAHALISI KUHUSIANA NA UCHAGUZI WA UBUNGE JIMBO LA KIJITOUPELE
Tume ya
Taifa ya Uchaguzi (NEC), inapenda kutaarifu Umma na Watanzania kwa ujumla kuwa
Jimbo la Kijitoupele lililoko Zanzibar ni miongoni mwa Majimbo hamsini(50)
ambayo yalitegemewa kufanya uchaguzi mkuu tarehe 25, oktoba,2015.
Hata hivyo
Jimbo hilo halikufanya uchaguzi wake wa Mbunge kutokana na hitilafu katika
karatasi za kupigia kura badala Wapiga kura walishiriki katika kumchagua Rais
wa Jamhuri ya Muungano.
Tume
imefikia uamuzi wa kutoa ufafanuzi huu kutokana na taarifa iliyochapishwa na
gazeti la MwanaHalisi toleo l Na.322 la Januari 18, 2016 katika ukurasa wake wa
mbele likidai “ NEC YAIBUA MAPYA” Habari hii si sahihi na inalenga kuupotosha
umma na kuleta uchochezi miongoni mwa Wananchi.
Kwa ujumla
maelezo yote yaliyopo katika taarifa hiyo yanaeleza kwamba, Tume imeanzisha
Jimbio jipya, kwa mujibu wa taarifa ya gazeti husika ni Jimbo la Kijitoupele –
Zanzibar.
Tume ya
Taifa ya Uchaguzi inapenda inasisitiza kuwa taarifa zilizotolewa na Gazeti la
MwanaHALISI siyo za kweli, ni za uongo, uzushi, uzandiki na uchochezi. Kufuatia
taarifa hiyo,Tume inapenda kutoa ufafanuzi ufuatao:
• Tarehe 13 Julai, 2015 Tume ya Taifa ya
Uchaguzi ilitoa taarifa kwa Vyombo vya Habari ikionesha Orodha ya Majimbo
yatakayofanya uchaguzi wa Mkuu wa tarehe 25 Oktoba, 2015 na Jimbo la
Kijitoupele lipo katika Orodha hiyo. Taarifa hii ipo katika tovuti ya Tume.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...