Matumizi ya dollar za kimarekani yamekuwa yakiongezeka siku hadi siku, hii imepelekea kuongezeka kwa thamani ya pesa hiyo kulinganisha na thamani ya pesa nyingine.
Miaka ya hivi karibuni kulikuwa na mkanganyiko na mikakati ya kurudisha thamani ya shilingi ya Kitanzania, lakini suala hili imekuwa si tatizo kwa nchi ya Tanzania pekee bali ni kwa nchi nyingi barani Afrika. hata hivyo JovagoTanzania imejaribu kutathmini thamani ya dola moja ya kimarekani na nchi kumi barani Africa ili kuitambulisha thamani yake ukiwa nje ya nchi.

Dolla moja imeonekana inathamani ya kipekee na kugundulika kuwa kwa Tanzania inaweza kusaidia kununulia muda wa maongezi na Vitu vingine vidogo vidogo, lakini kwa baadhi ya nchi nyingine kama Nigeria unaweza kupata hadi lita mbili za mafuta ya petroli.
Hata hivyo thamani ya pesa hutofautiana kati ya nchi na nchi, baadhi ya pesa zenye nguvu duniani ni pamoja na Kuwait dinar,Bahrain dinar,Oman rial, latvia lats, Uk Pound na Dola ya Kimarekani. Swali la kujiuliza pesa ya Tanzania ipo katika kiwango kipi!, ni kwa nini shilingi ya Kitanzania inashuka!, je kuna uwezekano wowote shilingi yetu ikapanda!

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...