Mpango
wa Kijamii wa Uzalishaji Salama ili kusaidia kaya masikini kupambana na
umasikini (PSSN) umefanikiwa kuwa na matokeo mazuri kwa kusaidia kaya
Milioni 1.1 nchini na kusaidia juhudi za serikali kupambana na
umasikini.
Hayo
yamefahamika wakati washirika wa maendeleo ambao ni Umoja wa Mataifa,
Benki Kuu ya Dunia, Serikali ya Uingereza kupitia kitengo cha Maendeleo
ya Kimataifa, Irish Aid, USAID, Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la
Sweden (SIDA) walipotembelea miradi ya maendeleo katika wilaya za
Unguja, Chamwino, Babati, Sumbawanga (Manispaa na Wilaya), Singida na
Hanang kwa kipindi cha siku tatu kuanzia Januari, 19 hadi 22.
Katika
Mpango huo ambao utekelezwaji wake unasimamiwa na Mfuko wa Maendeleo ya
Jamii (TASAF) unafanyika Tanzania Bara na Tanzania visiwani ukiwa na
lengo la kuzisaidia kaya masikini pesa za matumizi ili kukidhi mahitaji
ya kupata chakula pamoja na kuwawezesha kusaidia watoto wao kupata elimu
jambo ambalo linaonekana kuzaa matunda kwa maeneo mengi ikiwepo
Tanzania visiwani.
Serikali
ya Tanzania imekuwa ikisaidia na washirika wa maendeleo ili kupunguza
umaskini uliokithiri kwa wananchi wake na mwaka 2013 iliweka mpango wa
kusaidia kaya masikini 275,000 kwa kipindi cha miaka mitano na tangu
ianzishe mpango huo ilifanikiwa kusaidia kaya 275,000 kwa mwaka 2013
pekee katika wilaya nane nchini.
Na
mpaka kufikia sasa mpango huo umeshatoa malipo mara 12 na jumla ya kaya
masikini milioni 1.1 zimeshafaidika na mpango huo ikiwa ni kwa wilaya
161 na vijiji 9789 nchini.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...