NMB imekabidhi madawati 730 yenye thamani ya shilingi milioni 75 kwaajili ya shule za msingi 15 zilizopo wilayani Kiomboi – Singida huku kila shule ikipata madawati 50.
Msaada huo ni moja ya ushiriki wa benki katika maendeleo ya jamii na hivyo kuhakikisha kuwa jamii inayoizunguka benki hiyo inafaidika kutokana na faida wanayoipata. Katika mpango wake, NMB imetenga asilimia moja ya faida inayoipata baada ya kodi ambayo ni zaidi ya  shilingi bilioni 1 kwaajili ya kuchangia maendeleo ya wananchi ikiwemo kusaidia sekta ya afya na elimu.
 Shule zilizofaidika na msaada huo ni : Wala, Kisonga, Kigulu, Ujungu, Luzilukulu, Kiomboi, Lulumba, Isui, Tulya, Kitukuta, Mugela, Msai, Masagi, Kinkungu na Mtekente.
 Wakati huo huo Nmb imekabidhi vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi million 25 kwa mkuu wa mkoa wa singida.Vifaa tiba hivi vimetolewa kwaajili ya hospitali ya mkoa wa Singida ili kupunguza uhaba wa vifaa tiba ambao umekua ukiikumba Hospitali hii. Vitanda, magodoro na mashuka  ni miongoni mwa vifaa tiba vilivyo tolewa na NMB.
Akizungumza wakati wa makabidhiano Meneja wa Kanda ya Kati NMB  Bw.Stratoni Chilongola alisema “NMB inathamini wateja wake na ndio maana NMB imetenga Zaidi ya shilingi bilioni 1 kwaajili ya kuchangia maendeleo ya wananchi ikiwemo kusaidia sekta ya afya na elimu. Kiasi hiki kinatufanya kuwa benki ya kwanza katika kuchangia maendeleo ya jamii kuliko benki yoyote hapa nchini.”
Hafla hiyo ya makabidhiano iliyofanyika katika viwanja vya hospitali ya mkoa Singida iliwagusa wananchi wengi ambao wameshukuru uwepo wa tawi  NMB Mkoani Singida.
Afisa Elimu wa Wilaya  ya Kiomboi Clement Berege (kushoto) akipokea msaada huo
 Wanafunzi wakiwa na madawati hayo
 Wanafunzi wakipeleka madawati madarasani

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...