Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia,
Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla.
Serikali haitokuwa tayari kuwaona watumishi wa umma wachache wakinufaika na kufaidi pesa za walipa kodi hususani wa kipatao cha chini na wale maskinini.
Hayo yamesema wilayani hapa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla alipokuwa akiwahutubia
wananchi wa wilaya ya Nzega mkoani Tabora.
Dkt. Kigwangalla alisema serikali ya awamu ya tano inawataka
watumishi wote nchini kufanya kazi za kuwahudumia wananchi na kuacha uzembe
kwani awamu hii haiwezi kuwavumilia watumishi wa namna hiyo.
“Serikali haitowavumilia watumishi wazembe, hivyo tutaendelea
kuwafungia mageti na kuwashughulikia wale wazembe, tunataka watumishi wa umma
wafanye kazi ya kuwahudumia wananchi kwa ufanisi, mtumishi akizembea
tutamtumbua majipu, akichelewa tunamfungia geti na akiiba tunafilisi pamoja na
kumpeleka jela,hii ndiyo serikali ya hapa kazi tu,” alisema Dkt. Kigwangalla.
Aidha alisema serikali ya awamu ya tano inataka kero za wananchi
zifanyiwe kazi na kutekeleza ahadi zote za ilani ya uchaguzi ya ccm
zinatimizwa.
“Hatutomuonea mtu,lakini tutafanyia kazi pale penye
matatizo,tunataka Tanzania mpya ya mwaka 2015 inakua,hatutaki hadithi wala
ahadi,” alisema naibu waziri.
Hata hivyo aliwataka wazazi wote wenye watoto wenye umri wa kwenda
shule kuwapeleka watoto wao kuanza masomo kwani elimu kwa sasa ni bure na
hakuna michango yoyote.
“natoa wito kwa walimu wote wasitoze michango yeyote wala ushuru
kwa wazazi wanaowapeleka kuwaandikisha watoto shule kwani shule zimepatiwa pesa
za kuendeshea shule hizo,” alieleza Dkt. Kigwangalla.
Dkt. Kigwangwalla aliwakumbusha watumishi wa umma kujipanga na
kama watagundulika ni majipu bali hawatosita kuwatumbua hadi kina kitoke,usaha
na damu kutoka bila huruma.
Kazi nzuri mh, ila tungefurahi ungetupa updates za Dr mwaka
ReplyDelete