Afisa Uhusiano na Matukio wa Airtel, Dangio Kaniki (wa 3 kushoto) akimkabidhi Kanizio Annatory (katikati) ambaye ni miongoni mwa vijana waliowezeshwa na  mpango wa Airtel Fursa “Tunakuwezesha” mashine na vifaa vya kuoshea magari pamoja na sehemu ya kisasa ya kufanyia biashara, akishuhudiwa na ndugu zake pamoja na wafanyakazi wa Airtel katika hafla iliyofanyika kijiji cha Kamnazi mkoani Kagera.
 Afisa Uhusiano na matukio wa Airtel, Dangio Kaniki (kwanza kulia) pamoja na wafanyakazi wa Airtel wakimwonesha Kanizio Annatory (wa pili kushoto)  sehemu ya kisasa ya kuosha magari aliyowezeshwa na  mpango wa Airtel Fursa “Tunakuwezesha” baada ya kukabidhiwa mashine na vifaa vya kuosha magari katika hafla iliyofanyika kijiji cha Kamnazi mkoani Kagera.
Mwanzoni mwa wiki hii Airtel kupitia mpango wake wa Airtel Fursa  iliweza kufika  katika  kijiji cha  Kumnazi wilayani Ngara mkoani Kagera  na kumfikia Kijana  Kanizio Annatory anayejishughulisha na   biashara ya kuosha magari, kwa kumpatia vifaa na kufanyiwa ukarabati wa eneo lake la kazi . Vijana wengi wanaamini maisha mazuri na fursa za kiuchumi zinapatikana mjini, lakini kwa Kijana Kanizio kupita kwa barabara katika kijiji hiki ni fursa adhimu kwake.

Airtel Fursa  umelenga katika kuwezesha vijana  wajasiriamali hapa nchini kwa kutoa msaada kwa vijana ambao wanaonyesha juhudi ya kujikomboa na changamoto za maisha katika Jamii zinazowazunguka kwa kuwapatia vitendea kazi na kutoa mafunzo ya biashara ya ujasiriamali. Airtel Fursa ni moja ya sehemu ya utekelezaji wa wajibu wa Airtel  katika kurudisha sehemu ya faida wanayoipata kwa jamii ili kukidhi matakwa ya kiuchumi, na kuunga mkono jitihada za serikali katika kubadilisha maisha ya wananchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...