Mwenyekiti wa Bodi Jukwaa la Katiba Tanzania Bw. Deus M. Kibamba akiwatambulisha wajumbe wa Jukwaa hilo kwa Waziri wa Katiba na Sheria Mh. Dkt. Harrison Mwakyembe walipofanya nae kikao kuhusu mwelekeo mpya wa mchakato wa utungaji wa Katiba Tanzania. Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara ghorofa ya nane jijini Dar Es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi Jukwaa la Katiba Tanzania Bw. Deus M. Kibamba akimuelezea Waziri wa Katiba na Sheria Mh. Dkt. Harrison Mwakyembe umuhimu wa kumalizia suala la Katiba Mpya ambayo ni muhimu katika Taifa la Tanzania. Maelezo hayo yametolewa na Mwenyekiti huyo katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara ghorofa ya nane jijini Dar Es Salaam.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...