Na Bashir
Yakub.
Mara kadhaa tumeeleza
mambo mbalimbali ya kisheria kuhusu mikopo , waomba mikopo na
watoa mikopo. Haki
na wajibu ni
vitu ambavyo mara
nyingi vimeguswa. Hii ni
kwasababu eneo hili
ni katika maeneo
tata.
Ni tata kwa pande zote yaani
taasisi za fedha halikadhalika wachukua
mikopo. Iko sintofahamu
nyingi hasa kwa
wachukua mikopo. Mara nyingi
hawa hujikuta katika
matatizo na wakati
huo eti ndio
hufahamu haki na
wajibu wao.
Baada ya tatizo
kutokea ndipo hujua
walitakiwa kufanya nini huko
nyuma. Bahati mbaya muda huo huwa
wamechelewa tayari.
1.SUALA NA
KUWA NA MKE/MME WAKATI WA
KUCHUKUA MKOPO.
Wakati wa kuchukua
mkopo ni wakati
ambao taasisi inayotoa
mkopo humtahini ( interview) mchukua
mkopo. Kila taasisi yaweza
kuwa na maswali
ambayo yana tofauti na
taasisi nyingine. Maswali
hutokana na na taarifa ambazo taasisi ingependa kujua
kutoka kwa mchukua
mkopo.
Hata hivyo pamoja
na utofauti huo bado
yapo maswali ya
msingi ambayo kila taasisi
utakayoenda kuchukua mkopo
ni lazima utaulizwa.
Haya ni yale
yatokanayo na sheria zinazohusu masuala
ya mikopo. Ni maswali
yanayofanana( common questions).
Moja ya maswali
haya ni swali
hili la kutaka
kujua kama muomba
mkopo ana mwenza kwa
maana ya mke
au mme. Hili
ni swali la
kisheria ambalo lina
athari na matokeo
ya kisheria kama
tutakavyoona hapa .
2.UPI UMUHIMU
WA KUJUA IWAPO MWOMBA MKOPO
ANA MME/MKE.
Hii ni kwasababu
unapochukua mkopo mara
nyingi hutakiwa kuweka
rehani. Na rehani
inayokubalika huwa ni
mali isiyohamishika ambayo
ni nyumba au kiwanja. Na
mara nyingi nyumba au
kiwanja ni mali
ambazo huhesabika zinamilikiwa
kwa pamoja kati ya mme na
mke ikiwa wameoana.
Kwa maana si
ruhusa kwa mmoja
wa wanandoa hao kuweka
rehani mali hizo
bila mwingine kuridhia. Na ikitokea
kuwa mmoja hakuridhia basi
hupata haki ya kusitisha
mali hiyo kuhusishwa
katika mkopo.
Hatua hiyo inaweza
kuwa hasara kwa
mtoa mkopo. Basi kutokana
na hilo huibuka umuhimu mkubwa wa
kujua iwapo mwomba
mkopo ana mke/mme.
KUSOMA ZAIDI
sheriayakub.blogspot.com
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...