Na. Atley Kuni- Afisa habari Mwanza.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella amesema ifikapo tarehe 30. Mei, 2016 endapo
viongozi wa Wilaya za mkoa huo watakuwa bado wanakabiliwa na Ugonjwa wa Kipindupindu
katika wilaya zao basi wajiandae kuwajibika.
Alitoa kauli hiyo wakati akizungumza kwenye kikao cha kujitambulisha kwenye ukumbi wa ofisi
ya mkuu wa Mwanza mara baada yakuwasili mkoani humo na kuanza kazi mara moja.
Mongella alisema moja ya jambo lililonikera nikuona mkoa huo bado unakabiliwa na adha ya
kipindupindu huku Wakuu wa Wilaya, wakurugenzi na wataalam wakiwa hawana mipango
madhubuti yakutokomeza janga hilo “sasa tutaanza Operesheni maalum ijulikanayo Tukomeza
Kipindupindu Mkoa wa Mwanza kuanzia tarehe 01 Aprili,2016 na hatutakuwa na simile na
yeyote atakayetukwamisha” alisema na kusisitiza “Nina Machinery zote kwa nini nishindwe?
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...