Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (wa pili kutoka kulia) akikata utepe kuashiria ufunguzi wa mgodi. Wa kwanza kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Zelothe Stephen
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akiwasili katika mgodi wa dhahabu wa Cata Mining. Kulia ni Mkurugenzi wa mgodi huo, Mahuza Nyakirang’ani.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akikagua shughuli zinazoendelea mgodini hapo. Kushoto kwake ni Meneja wa mgodi huo, Peter Bourhill na kulia kwake ni Mkurugenzi wa mgodi,  Mahuza Nyakirang’ani.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akisalimiana na baadhi ya wananchi kutoka vijiji vya jirani na mgodi wa Cata Mining waliohudhuria mkutano wake wa hadhara ili kujadili masuala mbalimbali.
 Meneja wa mgodi wa Cata Mining, Peter Bourhill akimweleza jambo Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alipokua akikagua mgodi huo. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa mgodi,  Mahuza Nyakirang’ani.

Prof. Muhongo aagiza Malipo ya Ushuru wa Huduma yafanyike hadharani
Serikali imeagiza ulipaji wa ushuru wa huduma unayofanywa na migodi mbalimbali nchini ufanyike hadharani ili kila mwananchi aelewe kiasi kilicholipwa.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alitoa agizo hilo hivi karibuni alipofanya ziara kwenye mgodi wa dhahabu wa Cata Mining uliopo katika kijiji cha Kataryo, mkoani Mara ambapo vilevile alikagua shughuli za mgodi huo na kuweka jiwe la msingi.Profesa Muhongo alisema ili kuondoa hali ya sintofahamu pamoja na kuongeza uwazi na utekelezaji sahihi wa miradi kutokana na fedha zitokanazo na malipo ya ushuru wa huduma, ni lazima ulipaji huo wa ushuru husika ukashuhudiwa na kila mwananchi.

Aliongeza kwamba wananchi wanapaswa kushirikishwa katika kuibua miradi itakayotekelezwa kwa kutumia fedha hizo za ushuru wa huduma.“Wananchi wanapaswa kuelewa ni kiasi gani kimelipwa; na hiyo haitoshi inatakiwa washirikishwe kwenye matumizi ya fedha hiyo.”

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...