Mkuu
wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema (katikati) akimpima uzito mtoto
Shafii Haji (mwaka mmoja na nusu) mkazi wa Kibugumo Darajani, kama
ishara ya kuzindua kambi ya huduma za upimaji afya kwa watoto walio na
umri chini ya miaka mitano iliyofadhiliwa na Umoja wa Watu kutoka
Bengali, India wanaoishi Tanzania (Bango Sangho) katika shule ya Msingi
Kibugumo iliyopo Kigamboni jana jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mratibu
wa kambi hiyo kutoka Kliniki ya Al Hilal, Dk. Ali Mzige, Mbunge wa
Jimbo la Kigamboni, Dk. Faustine Ndungulile (wa kwanza kulia) pamoja na
Muuguzi wa Zahanati ya Kibugumo, Agnes Mokiwa (wa pili kulia)
wakishuhudia tukio hilo.
Meza
kuu kwenye uzinduzi wa kambi ya upimaji afya kwa watoto walio na umri
chini ya miaka mitano iliyofadhiliwa na Umoja wa Watu kutoka Bengali,
India wanaoishi Tanzania (Bango Sangho) katika shule ya Msingi Kibugumo
iliyopo Kigamboni jana jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Mratibu
wa kambi hiyo ya upimaji kutoka Kliniki ya Al Hilal, Dk.Ali Mzige,
Mwenyekiti wa Umoja wa Jamii ya watu kutoka India, Bengali waliopo
Tanzania (Bango Sangho), Kunal Banerjee, Mwalimu Mkuu wa Shule ya msingi
Kibugumo, Mzamilo Ally, Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia
Mjema pamoja na Mbunge wa Jimbo la Kigamboni, Dk. Faustine
Ndungulile.(Picha na Zainul Mzige wa Modewjiblog).
Mbunge
wa Jimbo la Kigamboni, Dk. Faustine Ndungulile akisisitiza jambo kwenye
uzinduzi huo kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia
Mjema kutoa nasaha katika ufunguzi wa kambi hiyo.
Mkuu
wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema akitoa neno la ufunguzi wa kambi ya
upimaji afya kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano iliyofadhiliwa
na Umoja wa Watu kutoka Bengali, India wanaoishi Tanzania (Bango Sangho)
katika shule ya Msingi Kibugumo iliyopo Kigamboni jana jijini Dar es
Salaam.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...