Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kulia) akisisitiza jambo kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Kuwait Mhandisi Yousef Al Fozan , (kushoto) aliyeongozana na maofisa wake wakati walipowasili ofisini kwake jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kusaini makubaliano ya safari za Anga baina ya Tanzania na Kuwait. Wapili kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya kati wa Wizara hiyo,Balozi Abdallah Kilima na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ua Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Hamza Johari.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Kuwait ,Mhandisi Yousef Al Fozan (kushoto) wakisaini hati za makubaliaono ya Usafiri wa Anga baina ya Kuwait na Tanzania , hafla hiyo ilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam, leo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Kuwait ,Mhandisi Yousef Al Fozan (kushoto) wakibadilishana hati za makubaliaono ya Usafiri wa Anga baina ya Kuwait na Tanzania , hafla hiyo ilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam, leo.


Maana yake ni nini makubaliano ya anga kati ya Kuwait na Tanzania, kwa sababu habari imejaa picha nyingi lakini haielezei mfano labda shirika la Etihad watakuwa wanafanya safari zaidi Tanzania n.k msomaji wa Globu anakuwa hajafaidika na habari hii zaidi ya kuona viongozi wakitia saini mkataba.
ReplyDelete