MBUNGE wa Viti  Maalum kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Vicky Kamata (Viti maalum CCM) amesema kwamba amejisikia furaha na ana kila sababu ya kuiomba kampuni ya Msama Promorions kutimiza ahadi yake ya kulipeleka  Tamasha la Pasaka mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Alisema kuwa mbali na burudani naamini kuwa hata wananchi watanufaika na Tamasha hilo kwa ujumbe  kwa wakazi wa Kanda ya Ziwa kuhusiana na mauaji ya walemavu wa ngozi 'albino' pamoja na vikongwe.

Kwa kweli mauaji hayo yanatokana na imani ya kishirikina lakini kwa tamasha hili ambalo ni sawa na kutangaza injili kwa njia ya nyimbo itaweza kuvunja nguvu za kishetani na wananchi kumrudia mungu.

“Nimefurahishwa katika hili naamini nguvu ya mungu itaenda kutenda kazi yake hivyo ni imani yangu kuwa watu watabarikiwa kwa kuvunja nguvu ya shetani na watu kumrudia mungu ,” alisema Mbunge huyo ambaye pia ni msanii.

Aidha Mbunge huyo alisema angefurahi kama waimbaji ambao wametajwa katika tamasha hilo kama Rose Muhando, Bonny Mwaitege na Upendo Nkone wafike Geita na wamewaandalia mapokezi ya aina yake kwani wana idadi kubwa ya mashabiki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...