Mwenyekiti wa Madaktari bingwa wa ugonjwa wa Moyo, Robart Mvungi akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam leo kuhusia na mkutano utakaofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam Aprili 21 na 22 mwaka huu, Amesema kuwa Mkutano huo utakuwa kwaajili ya kutoa elimu kwa wananchi kuhusiana na ugonjwa wa Moyo ambao sio wa kuambukizwa.
Pia amesema kuwa mkutano huo utahudhuliwa na Madaktari bingwa ugonjwa wa moyo pia watatumia muda huo kuelimisha jamii ili kuweza kupunguza ongezeko la ugonjwa wa moyo hapa nchini.
Kushoto ni Daktari Bingwa ya moyo katika hospitali ya Mhimbili katika Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete, Ruben Muta, Mwaandaaji wa mkutano, Adeline Ndesanja na Daktari Bingwa ya moyo katika hospitali ya Mhimbili katika Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete,Tulizo Sanga.




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...