Katibu wa kamati maalum ya NEC, idara ya itikadi na uenezi CCM Zanzibar Bi, Waride Bakar Jabu akimkabidhi misaada Katibu mkuu wa ofisi ya makamo wa pili wa rais, Joseph Abdallah Meza kwa ajili ya kuwasaidia wahanga wa mafuriko waliopo kambi ya mwanakwere "C" Unguja.
Katibu wa kamati maalum ya NEC, idara ya itikadi na uenezi CCM Zanzibar Bi, Waride Bakar Jabu akikagua wahanga wa mafuriko katika kambi ya mwanakwere zanzibar.
Kambi ya kipindupindu iliyopo chumbuni Zanzibar.
CHAMA chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimewataka wananchi kuendelea kufuata kanuni na taratibu zinazotolewa na wataalamu wa kiafya ili kujikinga na maambukizi ya maradhi ya kipindupindu yaliyopo nchini.
Wito huo umetolewa na Katibu wa Kamati Maalum NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar, Waride Bakar Jabu katika ziara ya kuwatembelea na kuwafariji wagonjwa wa Kipindupindu wa kambi iliyopo Chumbuni Zanzibar, alisema endapo wananchi watafuata kanuni za kiafya itasaidia kutoweka ugonjwa huo kwa haraka.
Waride alisema CCM itaendelea kutoa misaada ya hali na mali kwa wagonjwa wa kipindupindu ili kusaidia serikali huduma za uendeshaji kwa wagonjwa hao.
“ Tunawaomba wananchi waendelee kuweka mazingira yao katika hali ya usafi sambamba na kutumia maji salama, vyoo kuwa visafi na wagonjwa wenye dalili za maradhi hayo kupelekwa haraka katika kambi za kipindupindu.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...