Mwalimu Tabitha James Rhobi ni mwaka mmoja sasa tangu ufariki tarehe 02.04.2015. Tunakukumbuka kwa wema,upendo na busara.
Umeacha pengo kubwa na tunaendelea kupata faraja kupitia neno la Mungu katika Zaburi 46.
na tunasema ahsante Mungu kwa kuendelea kutupigania
Unakumbukwa na Mumeo Lucas Matiku, wanao Chris, Cath, James na Happy. Pia kaka zako David, Samweli nao wanakukumbuka. Wifi zako Feada na Mariam wanakukumbuka.
Bila kusahau walimu wenzako wa shule ya msingi Jangwani Beach wanakukumbuka
Misa ya shukrani itafanyika siku ya Jumamosi tarehe 02.04.2016 saa 9:00 alasiri nyumbani kwa Marehemu Mbezi Africana
Ndugu jamaa, marafiki na majirani mnakaribishwa kwa ajili ya misa hiyo



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...