Mwenyekiti wa  Chama cha mchezo wa Chess Tanzania (TCA) Bw. Geofrey Mwanyika akiongea na waandishi wa Habari hawapo pichani kuhusu mashindano ya mtu mmoja mmoja ya ukanda wa Afrika 4.2 yajulikanayo kama (2016 Africa Zone 4.2 Individual Chess Championship). Yatayofanyika hivi karibuni Jijini Dar es salaam.
Katibu wa Chama cha Mchezo wa Chess Tanzania (TCA) Bw. Nurdin Hassuji ambaye pia ni Bingwa wa Taifa wa mchezo huo akiongea na waandishi wa Habari hawapo pichani kuhusu mashindano ya mtu mmoja mmoja ya ukanda wa Afrika 4.2 yajulikanayo kama (2016 Africa Zone 4.2 Individual Chess Championship), kulia ni Mwenyekiti wa  Chama hicho Bw. Geofrey Mwanyika. Picha zote na Ally Daud- BMT.

Na Ally Daud- BMT
MASHINDANO ya mchezo wa chessi yanayojulikana kama mashindano ya mtu mmoja mmoja ya ukanda wa Afrika 4.2 (2016 Africa Zone 4.2 Individual Chess Championship) yanatarajiwa kuanza  tarehe 23 mwezi huu mpaka tarehe 30 April mwaka huu  hapa jijini Dar es salaam.

Akizungumza hayo mbele ya waandishi wa habari Mwenyekiti wa chama cha mchezo huo nchini (TCA) Bw. Geofrey Mwanyika amesema kuwa michuano hiyo iyafanyika katika Hoteli ya Peacock jijini Dar es salaam Tanzania ikiwa mwenyeji wa mashindano hayo.

Aidha Bw. Mwanyika ameinisha nchi ambazo zimeleta washiriki wake ni Uganda, Kenya, Rwanda, Burundi, Djibout, Eritrea,Somalia,Ethiopia, Sudan Kusini na wenyeji Tanzania  “Jumla ya washiriki 32 watachuana katika mashindano hayo ambayo yamegawanyika katika makundi mawili ya Wanaume na Wanawake na kati ya nchi hizo ambazo zinashiriki Sudan na Seychells hazijathibitisha kushiriki”. Aliongeza Bw. Mwanyika.

Kwa upande wa Katibu wa TCA  Bw. Nurdin Hassuji ambaye pia ni Bingwa wa Taifa wa mchezo huo amesema kuwa zawadi za washindi ni Dola 4500  za Kimarekani ambazo zitagawanywa kwa watakaoshinda.

Aidha Bw. Hassuji amewataka wadau wa Michezo  na waandishi wa habari kujitokeza siku hiyo ili kuipa sapoti timu yao na kuutangaza mchezo ujulikane na kupendwa zaidi nchini.

Mbali  na hayo Bw. Hassuji amesema kuwa mchezo huo wameupa kipaumbele na kwenda kuufundisha mashuleni kwa sababu inawasaidia wanafunzi kuweza kufikiri kwa haraka zaidi na kufanya mwanafunzi awe mwepesi kwenye kupambanua mambo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...