Kamishna Msaidizi wa Madini, Kanda ya Kaskazini, Elias
Kayandabila akisisitiza jambo kabla ya ufunguzi wa masanduku
yenye bahasha za ahadi ya bei za madini yaliyopigwa mnada
katika Maonesho ya Tano ya Kimataifa ya Vito yaliyofanyika jijini
Arusha kuanzia tarehe 19 hadi 21, Aprili, 2016. Katikati ni Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO),
Zena Kongoi na kushoto ni mmoja wa Wakurugenzi wa Kampuni
ya Sky Associates Faisal Juma Shahbhai inayomiliki mgodi wa Tanzanite
One kwa ubia na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO).
Mkurugenzi wa Kitengo cha Uthaminishaji Madini ya Almas na
Vito, katika Wizara ya Nishati na Madini, Archard Kalugendo
akiangalia maombi ya ahadi za bei ya madini yaliyopigwa mnada
katika Maonesho ya Tano ya Kimataifa ya Vito yaliyofanyika jijini
Arusha kuanzia tarehe 19 hadi 21, Aprili, 2016. Wanaoshuhudia
ni Kamishna Msaidizi wa Madini, Uchumi na Biashara, Salim
Salim (Wa Pili kushoto), Wa Pili kulia ni Mkurugenzi wa Uthamini
wa Madini na Huduma za Kimaabara katika Wakala wa Ukaguzi
wa Madini Tanzania (TMAA), Mhandisi Gilay Shamika na wa
kwanza kulia ni Mthamini Almas wa Serikali, Edward
Rweyemamu.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Uthaminishaji Madini ya Almas na
Vito, katika Wizara ya Nishati na Madini, Archard Kalugendo
akionesha masanduku yenye bahasha za ahadi ya bei za madini
yaliyopigwa mnada katika Maonesho ya Tano ya Kimataifa ya
Vito yaliyofanyika jijini Arusha kuanzia tarehe 19 hadi 21, Aprili,
2016. Wanaoshuhudia ni Kamishna Msaidizi wa Madini, Uchumi
na Biashara, Salim Salim (katikati) na kulia ni Mkurugenzi wa
Uthamini wa Madini na Huduma za Kimaabara katika Wakala wa
Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA), Mhandisi Gilay Shamika.
Wadau mbalimbali walioshiriki Maonesho ya Tano ya Kimataifa
ya Vito yaliyofanyika jijini Arusha kuanzia tarehe 19 hadi 21
wakimsikiliza Mkurugenzi wa Kitengo cha Uthaminishaji Madini ya
Almas na Vito, katika Wizara ya Nishati na Madini, Archard
Kalugendo (hayupo pichani) wakati akitangaza matokeo ya
mnada wa madini uliofanyika katika Maonesho hayo.
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...