Kamishna Msaidizi wa Madini, Kanda ya Kaskazini, Elias Kayandabila akisisitiza jambo kabla ya ufunguzi wa masanduku yenye bahasha za ahadi ya bei za madini yaliyopigwa mnada katika Maonesho ya Tano ya Kimataifa ya Vito yaliyofanyika jijini Arusha kuanzia tarehe 19 hadi 21, Aprili, 2016. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Zena Kongoi na kushoto ni mmoja wa Wakurugenzi wa Kampuni ya Sky Associates Faisal Juma Shahbhai inayomiliki mgodi wa Tanzanite One kwa ubia na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO).
Mkurugenzi wa Kitengo cha Uthaminishaji Madini ya Almas na Vito, katika Wizara ya Nishati na Madini, Archard Kalugendo akiangalia maombi ya ahadi za bei ya madini yaliyopigwa mnada katika Maonesho ya Tano ya Kimataifa ya Vito yaliyofanyika jijini Arusha kuanzia tarehe 19 hadi 21, Aprili, 2016. Wanaoshuhudia ni Kamishna Msaidizi wa Madini, Uchumi na Biashara, Salim Salim (Wa Pili kushoto), Wa Pili kulia ni Mkurugenzi wa Uthamini wa Madini na Huduma za Kimaabara katika Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA), Mhandisi Gilay Shamika na wa kwanza kulia ni Mthamini Almas wa Serikali, Edward Rweyemamu.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Uthaminishaji Madini ya Almas na Vito, katika Wizara ya Nishati na Madini, Archard Kalugendo akionesha masanduku yenye bahasha za ahadi ya bei za madini yaliyopigwa mnada katika Maonesho ya Tano ya Kimataifa ya Vito yaliyofanyika jijini Arusha kuanzia tarehe 19 hadi 21, Aprili, 2016. Wanaoshuhudia ni Kamishna Msaidizi wa Madini, Uchumi na Biashara, Salim Salim (katikati) na kulia ni Mkurugenzi wa Uthamini wa Madini na Huduma za Kimaabara katika Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA), Mhandisi Gilay Shamika.
Wadau mbalimbali walioshiriki Maonesho ya Tano ya Kimataifa ya Vito yaliyofanyika jijini Arusha kuanzia tarehe 19 hadi 21 wakimsikiliza Mkurugenzi wa Kitengo cha Uthaminishaji Madini ya Almas na Vito, katika Wizara ya Nishati na Madini, Archard Kalugendo (hayupo pichani) wakati akitangaza matokeo ya mnada wa madini uliofanyika katika Maonesho hayo.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...