leo (JANA)  31/03/2016  Mkuu wa wilaya Iringa ambaye pia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa ameshiriki kwenye mazishi mazishi ya Mnywarwanda Jeannnete Mukashema aliyefariki kwenye ajali iliyotokea usiku Juzi. Bi Jeanette alikuwa akisafiri na mtoto wake ambaye naye aliumia kwenye ajali hiyo bado anaendelea na matibabu. 

Akizungumza Mh Kasesela alisema " Imeniuma sana kwani niliupokea mwili kwa mikono yangu tukiwa na waokoaji wengine alipo tolewa juu kwenye basi bado tukio hilo limo mawazoni mwangu na nguo zangu zikiwa na madoa ya damu , tulimpokea akiwa tayari amefariki. 

Kesho yake mtoto alipo zinduka akaanza kumtafuta mama yake nilipo mtembelea asubuhi, nilijua mama yake amekufa nilishindwa kumwambia leo alipo niona ameanza kulia amenikumbusha nikiwa miaka 11 nilipo ondokewa na mama yangu. lakini naamini yuko katika mikono salama, Mungu ni mwema baba yake na ndugu wengine wamekuj kutoka  Rwanda. BWANA AMETOA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE"

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. RIP Mama, poleni kwa familia hiyo, Kijana tunakuombea Mungu atakulinda. Richard Kasesera, you are such a great leader.
    Joshefu dar

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...