Gari lililobeba sanduku lenye mwili wa marehemu Onawembo Ngongo a.k.a Ndanda Kosovo, likiwasili kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar leo jioni tayari kwa mazishi.
Waziri wa Habari, utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Nape Nnauye akiweka shada la Maua kwenye kaburi la Marehemu Onawembo Ngongo a.k.a Ndanda Kosovo, wakati wa mazishi yaliyofanyika kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar jioni ya leo.
Sanduku lenye mwili wa Marehemu Onawembo Ngongo a.k.a Ndanda Kosovo,likishushwa kwenye nyumba yake ya Milele,makaburi ya Kinondoni jijini Dar leo jioni.
Mama wa Marehem Ndanda Kosovo akimshukuru Waziri Nape Nnauye pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kukubali mtoto wake kuzikwa katika ardhi ya Tanzania.
Baadhi ya Wafiwa wakiwa Makaburini tayari kushirik mazishi ya mpendwa wao Ndanda Kosovo.
Taratibu za Maziko zikiendelea makaburi ya Kinondoni jijini Dar.
Hapa ndipo mahala alipohifadhiwa Mwanamuziki Mkongwe wa Dansi hapa nchini, Marehemu Onawembo Ngongo a.k.a Ndanda Kosovo,amezikwa leo jioni katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar,ambapo Waziri mazishi hayo yameongozwa na Wazir Nape Nnauye,Mkuu wa Mkoa Paul Makonda,Wanamuziki,wasanii wa filamu,ndugu jamaa na marafiki kutoka sehemu mbalimbali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Rest in peace Ndanda Kosovo mjelajela origino, wamekula ya mbuzi wameota mapembe

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...