
Gari lililobeba sanduku lenye mwili wa marehemu Onawembo Ngongo a.k.a Ndanda Kosovo, likiwasili kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar leo jioni tayari kwa mazishi.

Waziri wa Habari, utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Nape Nnauye akiweka shada la Maua kwenye kaburi la Marehemu Onawembo Ngongo a.k.a Ndanda Kosovo, wakati wa mazishi yaliyofanyika kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar jioni ya leo.
Sanduku lenye mwili wa Marehemu Onawembo Ngongo a.k.a Ndanda Kosovo,likishushwa kwenye nyumba yake ya Milele,makaburi ya Kinondoni jijini Dar leo jioni.
Mama wa Marehem Ndanda Kosovo akimshukuru Waziri Nape Nnauye pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kukubali mtoto wake kuzikwa katika ardhi ya Tanzania.
Baadhi ya Wafiwa wakiwa Makaburini tayari kushirik mazishi ya mpendwa wao Ndanda Kosovo.
Taratibu za Maziko zikiendelea makaburi ya Kinondoni jijini Dar.
Hapa ndipo mahala alipohifadhiwa Mwanamuziki Mkongwe wa Dansi hapa nchini, Marehemu Onawembo Ngongo a.k.a Ndanda Kosovo,amezikwa leo jioni katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar,ambapo Waziri mazishi hayo yameongozwa na Wazir Nape Nnauye,Mkuu wa Mkoa Paul Makonda,Wanamuziki,wasanii wa filamu,ndugu jamaa na marafiki kutoka sehemu mbalimbali.
Rest in peace Ndanda Kosovo mjelajela origino, wamekula ya mbuzi wameota mapembe
ReplyDelete