Kwa mujibu wa imani na filosofia ya sanaa ya Yoga, Kufunga ama kushinda Zaidi ya masaa 24 bila kula chakula ni moja ya mbinu adilifu katika  sanaa hii yenye mafunzo na tiba asilia yenye  zaidi ya karne moja. Kufunga, kunywa maji na mbinu za mazoez yenye chimbko na mikao ya wanyama ni misingi muhimu katika Sanaa hii ya mafunzo asilia ya mwanadam.
Katika somo la mafunzo ya Yoga, upo uthibiti wa kuamini kwamba mwei mchanga na mwezi mpevu unaathari kubwa sana katika ubongo wa mwanadamu kitabia na pia kimatendo. Ipo Imani kubwa sana kwa wana- Yoga au “Yogi” kuamini kwamba mwili wa mwanadam uwejengwa na asilimia 70% ya maji. Hivyo, kama jinsi mwezi unamvuto wa wimbi katika bahari ambayo husababisha maji kutoweka ufukweni kwa muda kadhaa wakati wa mwezi mchanga na mwezi mpevu, ndivyo hivyo jinsi mwili wa mwanadamu ambao unamaji asilimia 70% na kusababisha wimbi kama hilo lenye athari kubwa kitabia na vitendo kwa watu wengi kipindi hicho.
Kutokana na filosofia ya Yoga inaamini, siku tatu kabla na siku tatu baada ya mwezi mchanga au mpevu, kunamvutano mkubwa wa wimbi la maji mwilini kuvutwa katika  ubongo wa mwanadamambao usababisha athari kubwa kimawazo na hata kivitendo.  Athari hiyo ni kama vile kutokuwa mtulivu, hasira, uchokozi wa bila sababu, na pia tabia za ajabu ikiwemo hata ukatiri wa vitendo. Katika kipndi hiki cha mwezi mpevu hutokea matukio mengi ya kinyama, kama vile ghasia n ahata mauaji sababu wengi wa waathirika ushawishiwa kufanya uovu kutokana na mvuto wa hilo wimbi na mwezi mpevu au mchanga.
Mwezi mchanga”Ekadashi”  au mwezi mpevu “Purnima” katika lugha ya “Sanskrit” ni moja ya siku muhimu sana katika folosofia ya Yoga kuhakikisha unatuliza na kupoza fikra za mtu kupitia Sanaa hii ya kutafakari na kufunga kuimarisha udhaifu wa athari ya mwezi katika ubongo wa mwanadam.
Mseomo ujulikanao “Lunar” ina fananishwa sana na kile kiitwacho”Lunatic” ambao ni athari hizo zilizoelezewa hapo juu kuhuku madhara ya mwezi mpevu au mchanga na jinsi unavyo sababisha ghasia katika fikra na wengi kitabia.
Unapokuwa unafunga katika kipindi hicho cha siku tatu kabla au tatu baadae, ni husababisha tumbo kavu kuvuta maji mwilini inayo sababishwa na mwezi “Lunar”, na badala yake kuweza kumiliki hali ya usawa  na uadilifu kitabia.
Hivyo tu kwa muktasari wa Sanaa ya Yoga,  kufunga ni afya na muhimu sana kwa kuzingatia ubora wa mawazo na maamzi ya busara katika kile kipindi kiitwacho “ Lunar”.
Baada ya kufunga masa 24, inashauriwa kisaa ya Yoga kunywa angalau lita moja na nusu ya maji vuguvgu ya chumvi na ndizi iliyo wiva sana kusafisha tumbo baada ya kufunga. Pia ni njia fasaha ya kutakasa utumbo mkuu wa chakula mara moja kwa mwezi. Baada ya hapo, ndipo pale mafunzo ya mazoezi ya yoga “Asanas” hufanya hali ya mwili kuwa imara na afya njema na akili kuwa timamu pia.

 Hii ni moja ya kurasa za somo la Yoga na maisha kiujumla kutoka katika daftari la mwalimu wa Yoga, Sensei Rumadha Fundi, mkufunzi wa Sanaa ya Yoga mwenye kushikilia ngazi ya juu kabisa ya masomo hayo baada ya kuhitimu masomo Na Mchanga  katika vyuo vya tawi hilo huko Sweden na hatimaye  kwa master wa Yoga “Guru, Shrii Shrii AnandaMurtiji” huko Calcutta, India, 1987.

 Sensei Rumadha Fundi katika zoezi la Yoga. Chini ni binti yake ambaye naye anafuata nyayo za baba yake kwenye mazoezi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Fred Macha hapo kimyaaaaaaaa!!!! mwenyewe Sensei Rumadha mtoto wa kitovu jiji Karikoo akichambua kwa undani masuala ya Yoga,Big Up Sensei Rumadha

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...