Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Madini, Profesa James Mdoe (katikati) akiwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, wakisikiliza maelezo kutoka kwa Meneja wa Mgodi wa Tanzanite, Emmanuel Mbise ulioko Kitalu B, Mirerani. Mgodi huo unamilikiwa na Mchimbaji Mdogo, Ester Ndosi.
Kamishna Msaidizi wa Madini, Kanda ya Kaskazini, Elias Kayandabila, akifafanua jambo kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, walipotembelea Mgodi wa madini ya Tanzanite wa Franone uliopo Kitalu D, Mirerani. Wa kwanza Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, anayeshughulikia Madini, Profesa James Mdoe.
Kaimu Kamishna wa Madini, Mhandisi Ally Samaje (Kulia), akimwonyesha Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Madini, Profesa James Mdoe (Kushoto), namna Kiberenge kinavyofanya kazi ya kushusha watu na vifaa chini ya ardhi kunakochimbwa madini ya Tanzanite, wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini katika Mgodi wa Tanzanite One uliopo Mirerani, hivi karibuni.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...