Theresia.S.Assey
Kuz: 27.01.1943 – Kuf: 28.03.2016


Familia ya Bw. Stephen Philiph Assey wa Kijitonyama Dar es Salaam, inayo heshima kubwa kutoa shukrani za dhati kabisa kwa ndugu, jamaa na marafiki ambao walishiriki kwa namna moja ama nyingine kufanikisha msiba, mazishi na hatimaye matanga ya Mama/Bibi yao mpendwa, Theresia.S.Assey, aliyefariki dunia alfajiri ya  Jumatatu  ya 27th March, Kijitonyama Dar es Salaam na kuzikwa Makaburi ya Kinondoni, Alhamisi ya 30th march , 2016.

Kwa vile waliwotuunga mkono na kutufariji wakati wa kipindi hiki kigumu cha msiba huu mkubwa ni wengi na ni vigumu kuwataja wote kwa majina, Familia, inapenda kwa heshima na taadhima nyingi kutoa shukrani za jumla ikiwaomba wote mkubali kuzipokea kwa moyo ule ule kama mlivyotuunga mkono. Mmetufariji sana, mmekesha nasi, mmeshinda nasi, nyote mmekuwa kimbilio salama kwetu wakati wa kipindi hiki kigumu. 

Mmeonesha upendo wa kweli kweli kwetu kama Familia na kwa Mama/Bibi  yetu Theresia ambaye angerejea kwenye uzima tena, naye bila shaka yoyote angetoa shukrani za dhati ya moyo wake.

Hata hivyo, tunapenda kutoa shukurani kwa makundi machache ya marafiki ambao mchango wao utabakia kwenye nyoyo za wazazi na familia yetu  tukianza na majirani na marafiki wa karibu wa Familia walioko Dar es Salaam, Moshi, Arusha, Mbeya na kwingineko  na nje ya Afrika Mashariki, ambao michango yao kamwe haitasahaulika.

Familia pia inapenda kushukuru Kanisa Katoliki la Mwananyamala chini ya Paroko wake na wanajumuia ya Mtakatifu Clara Mtaa wa Makumbusho Dar Es Salaam, Uongozi na Washarika wa  Biblical Counselling and Intercession Centre(BCIC)-Mbezi Beach.  kwa huduma kubwa za kiroho wakati wa msiba huo mkubwa uliotufika.

Familia vile vile inapenda kutoa shukrani za dhati kabisa kwa Madaktari, na kwa Wauguzi na  wa Hospitali za Kairuki,  Regency hospital, Abass medical clinic na Muhimbili Dar es Salaam kwa juhudi zao za dhati za kutaka kuokoa maisha ya Mama yetu.

Aidha, tunatoa shukrani kwa wafanyakazi  wa Msajili wa Vyama Vya Siasa,Mahakama ya Tanzania  Airtel-Nokia, Wafanyakazi wa Chuo kikuu Cha Ardhi, NMB-Mbezi Branch na CRDB  Bank kwa  michango yenu, ilitufariji na tutaendelea kukumbuka ukarimu wenu daima. 

Mwisho Tunawashukuru nyote mlioweza kufika nyumbani Kijitonyama na Makaburini Kinondoni  kumhifadhi Bibi Tere.  Hatuna cha kuwalipa, Mungu atawalipa.

“Mathayo 5:8:-Heri wenye moyo safi; Maana hao watamwona Bwana”

Mungu awabariki  sana

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Rest in eternal peace mom...

    ReplyDelete
  2. Rest in eternal peace mom..will always love u

    ReplyDelete
  3. Rest in eternal Peace mom...we will always have u in our hearts.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...