Wizara ya Maji na Umwagiliaji imetia saini ya makubaliano maalum (MoU) na Sekretarieti ya AMCOW ya kukubali Tanzania kuwa mwenyeji wa Mkutano Mkuu wa 10 wa Baraza la Mawaziri wa Maji wa Afrika (AMCOW) na Maadhimisho ya 6 ya Wiki ya Maji ya Afrika.

Makubaliano hayo yalisainiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Inj. Mbogo Futakamba na Mtendaji Mkuu wa AMCOW, Bai Mass Taal leo mchana, katika Mkutano na Waandishi wa Habari uliofanyika katika Makao Makuu ya Wizara hiyo, Ubungo Maji.

Mkutano huo na Maadhimisho hayo ya Kimataifa yatafanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam kuanzia tarehe 18-22, Julai na Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Inj. Mbogo Futakamba akizungumza, kushoto ni Mtendaji Mkuu wa AMCOW, Bai Mass Taal na kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali za Maji, Dkt. George Lugomela.
Mtendaji Mkuu wa AMCOW, Bai Mass Taal akizungumza, pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Inj. Mbogo Futakamba.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Inj. Mbogo Futakamba na Mtendaji Mkuu wa AMCOW, Bai Mass Taal wakisaini hati za makubaliano huku wakishuhudiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali za Maji, Dkt. George Lugomela.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...