Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) yatoa mkopo wa 890 Milioni kwa wakulima wa zao la mpunga wanaojishughulisha kilimo cha umwagiliaji katika Kijiji cha Mkula wilayani Kilombero ili kuongeza tija na uzalishaji wa zao la mpunga.
Hayo yaliwekwa bayana na Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara wa TADB, Bw. Robert Paschal wakati wa warsha ya wakulima wadogo zaidi ya 340 wa Mkoa wa morogoro iliyofanyika katika Ukumbi wa Mazingira Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.
Bw. Paschal alisema lengo la mkopo huo unaowanufaisha zaidi ya wakulima 350 ni kuongeza tija na uzalishaji wa mpunga ili Kusaidia upatikanaji wa utoshelezi na usalama wa chakula ambao ni endelevu nchini Tanzania na kuchagiza na kusaidia Mapinduzi ya Kilimo kutoka kilimo cha kujikimu kwenda cha kibiashara ili kuchangia kwenye ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini.
“Mkopo huu na mengine tunayotoa imelenga kuongeza tija na uzalishaji katika kilimo ili kusaidia kukabiliana na mapungufu hayo na kuhuisha upatikanaji wa mikopo katika sekta ya kilimo ili kuleta mapinduzi katika kilimo nchini,” alisema Bw. Paschal.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...