Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo leo imetangaza kuufungia wimbo na video ya Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya, Snura Mushi unafahamika kwa jina la CHURA kutokana na kutokuwa na maadili ya Mtanzania.

Wimbo huo pia umezuiwa kutumbuizwa mahala popote na kufungiwa kuchezwa kwenye redio na runinga nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo, Mkuu wa Kitengo cha mawasiliano wa wizara hiyo, Zawadi Msalla, amewaonya watu kutousambaza wimbo huo kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo WhatsApp na Istagram na kuongeza kuwa wale watakaokiuka agizo hilo watashtakiwa kwa kutumia sheria ya makosa ya mtandao.

Pia Wizara hiyo, imesitisha maonyesho yote ya hadhara ya Msanii huyo, mpaka pale atakapo kamilisha taratibu za usajili wa kazi zake zote kwa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA).

Serikali imewataka wanasii mbali mbali nchini, kujiuliza mara mbili kabla ya kubuni kazi zao za sanaa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 04, 2016

    Mambo ya "Cheza kibobmale" hayo!!! chura karukaruka chura!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...