Na Jacquiline Mrisho- MAELEZO

Maji ni rasilimali muhimu kwa maisha ya viumbe vyote pamoja na maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Kiwango cha maendeleo ya jamii yoyote, ubora wa afya na mazingira kwa ujumla vinategemea kuwepo kwa maji yakutosha na yenye ubora unaotakiwa.

Maji yana mchango mkubwa sana katika maendeleo ya jamii kwa kuwa hutumika kwa matumizi mbalimbali kama vile kuzalisha umeme,kupika, kuoga na kufua nguo, katika ujenzi na kusaidia maisha ya viumbe hai, matumizi ya viwandani pamoja na kilimo hivyo usimamizi na utunzaji wake lazima uzingatiwe.

Serikali ina malengo ya kuwapatia maji wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, Mkoa wa Pwani, Kibaha pamoja na Bagamoyo kwa asilimia 100 ifikapo mwaka 2025.Hakika aja ya mja hunena, muungwana ni vitendo. Hii imethibitika kuwa kweli Serikali ya Awamu ya Tano inajali watu wake hasa wa hali ya chini kama Rais John Pombe Magufuli ambavyo hupenda kuwaita wanyonge. Watu wengi wanahitaji kuwa na maji ya bomba lakini uwezo wa kuunganisha ulikuwa mgumu kwani gharama wengi waliiona kuwa ni kubwa sana.

Kwa kulitambua hilo Serikali imeamua kuingia gharama za kuwaunganishia maji wateja wake na wenyewe watalipia kidogo kidogo gharama hizo. Hili ni jambo la kuungwa mkono sana.Hapa tunamsikia mkazi wa Mbweni, Jijini Dar es Salaam, Bi Fatuma Iddi akisema,“Kwa kweli serikali hii imetukumbuka, mimi nilishapoteza matumaini ya kupata maji kwangu kwani sikuwa na uwezo wa kulipa malaki hayo kwa ajili ya kuunganishiwa. Lakini kwa kulipia kwa awamu hilo nitalimudu. Heko Mhe. Rais Magufuli kwa kutujali hasa sisi wanyonge.”

Takwimu zilizotolewa na Ofisi ya Mkoa wa Dar es Saalam zinaeleza kuwa Mkoa unapata maji kutoka katika mito na visima ambapo eneo kubwa la Mji huo linahudumiwa na Kampuni ya Maji Safi na Maji Taka (DAWASCO) ambayo imepewa mkataba na Mamlaka ya Maji Safi na Maji taka Dar es Salaam (DAWASA) na kwa maeneo yasiyo na mtandao wa DAWASA hupata maji kutoka kwenye visima vinavyoendeshwa na vyombo vya watu binafsi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...