Na Eliphace Marwa - Maelezo

Meya wa Jiji la Dare s Salaam Mh. Issaya Mwita ameipongeza klabu ya Yanga kwa kunyakua ubingwa huo kwa mara ya Ishirini na Sita tangu kuanzishwa kwa mashindano ya ligi kuu hapa nchini.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari Mh. Mwita amesema ushindi wa Klabu ya Yanga umeliwezesha Jiji la Dar es Salaam kuendelea kupata sifa katika medani ya Kitaifa na Kimataifa kutokana na ushiriki wa klabu hiyo katika mashindano ya kimataifa.

“Ninaiomba klabu ya Yanga kuthamini ubingwa wao kwa kuonyesha viwango vya kimataifa ili kulifanya jiji hili kuwa chuo cha mafunzo ya mchezo wa mpira wa miguu,” alisema Mh. Mwita.

Aidha aliliomba Shirikisho la Mchezo wa MPira wa Miguu nchini (TFF) kuendelea kusimamia ligi kwa ustadi  zaidi ili kulingana na taratibu za mpira wa miguu kama zinavyoainishwa na Shirikisho la  Soka duniani (FIFA) pamoja na Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF).

“Naomba nitoe wito kwa wadau wote katika familia ya mpira wa miguu kushirikiana ipasavyo ili kufanya ligi yetu iwe miongoni mwa ligi bora barani afrika na Duniani kwa ujumla,” aliongeza Mh. Mwita.

Pia aliwapongeza wadhamini wote waliojitolea kusaidia ufadhili kwa vilabu vyote vilivyoshiriki ligi kuu na kuwataka waendelee kuwasaidia ili kuinua soka letu la bongo.

Aidha ameitakia klabu ya Yanga ya Jangwani maandalizi mema katika mchezo wa marudiano wa kufuzu hatua  za makundi ya kombe la Shirikisho la mpira wa miguu Barani Afrika (CAF) dhidi ya klabu ya Sagrada Esperance huko nchini Angola.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...