Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu ameshiriki kwenye Mkutano mkubwa wa Kimataifa, Women Deliver uliofanyika Copenhagen, Denmark tarehe 16-19 Mei, 2016. Mkutano huo ulihudhuriwa na wajumbe wanaokaribia 5800 kutoka nchi 169. 
 Akiwa kwenye mkutano huo, Mhe. Waziri Ummy Mwalimu alipata pia fursa ya kutembelea maonyesho yaliyokuwa yakifanyika sambamba na mkutano huo. Mhe. Waziri Ummy Mwalimu alipata pia fursa ya kufanya Kikao na washiriki wote kutoka Tanzania. 
Lengo la kikao hicho lilikuwa ni kupanga Mikakati ya kuyafanyia kazi kwa pamoja mambo yote muhimu yaliyojitokeza kwenye Women Deliver Conference. 
 Tanzania ilikuwa na washiriki zaidi ya 40 kutoka taasisi mbalimbali zinazohusiana na masuala ya wanawake wakiwemo wabunge, wanafunzi,NGOs na wadau wengine wa sekta zinazojihusisha na masuala ya wanawake.

Mbunge wa Babati, Mhe Pauline Gekal, Dkt. Neema Rusibamayila, Mhe. Ummy Mwalimu na Mhe. Dora Msechu, Balozi wa Tanzania kwenye nchi za Nordic na Baltic katika mjadala
 Mhe. Waziri alihudhuria pia East African Regional Caucus

Ni wakati wa maswali na majibu
 Mhe. Waziri alipiga picha ya pamoja na nyingine na washiriki kutoka Tanzania
 Mhe. Waziri alipiga picha ya pamoja na nyingine na washiriki kutoka Tanzania
Mhe. Waziri alitembelea pia banda la Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...